Wednesday 6 June 2007

Hatimaye WTM wametoa DUBIOUS address.


Baada ya kubainishwa kwamba address waliyotoa WTM huko Dagenham inatiliwa mashaka katika blog hii, leo hii wametoa address mpya ambayo pia ina utata kama zoezi ambalo wanakusudia kulifanya. Hatimae address yao imezaa address mbili kwa moja barking/dagenham kama inavyoonyesha kwenye tovotu yao, katika maisha yangu kukaa UK, sijawahi kuona address ina address mbili kwa moja, inadhihirisha wazi kwamba hii kampuni hawajui wanachokifanya na wanachokikusidia kukifanya, bali ni sehemu ya kitengo cha kuchukulia wafanyabiashara pesa zao bila kuwa na mantiki au taratibu za kuaminika katika kufanya zoezi hilo.


Hata hivyo leo hii WTM wametoa press release, ambayo inaongelea kuhusu zoezi hilo la ukaguzi wa magari, ambalo litaanza tarehe 06 June 2007, na siyo tarehe 14 MAy 2007 kama ilivyoelezewa hapo awali, walipoingia mkataba na TBS.

Kama tulivyoolezea hapo awali wafanyabiasha lazima, wapeleke malalamiko yao kwenye vyombo vya sheria hapa UK na huko Tanzania kupata uwazi wa huu utaratibu mzima wa hili zoezi gharamu ambalo mpaka muda huu, hakuna taratibu kamili ambayo iko wazi kwa wananchi, hususan kuhusu hili swala la gari kuwa MOT, inakua vipi tuwapelekee hawa jamaa kukagua gari hilo hilo.

Hii licence yao, kama wanvyodai wamepatiwa kuweza kuanzisha hili zoezi, lazima iangaliwe upya na malalamiko lazima yapelekwe VOSA uk, na vyombo vyengine husika vya kiserikali UK.


Mpaka hivi sasa sina Clue WTM ina maana gani kwa urefu ?? SAY NO DUBIOUS COMPANY SAY NO DUBIOUS DEAL

No comments: